Bondia Mtanzania Ibrahim Class Mgendera, anatarajia kutetea ubingwa anaoushikilia wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight dhidi ya bondia kutoka nchini Afrika Kusini

Pambano hilo la kimataifa la ngumi za kulipwa ambalo limedhaminiwa na kampuni ya simu ya Vodacom PLC pamoja na kampuni ya Azam, litafanyika jijini Dar es Salaam Novemba 25 2017 kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Mgendera anashikilia ubingwa wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight”ambao alioutwaa nchini Ujerumani tarehe 1 Julai, 2017 kwa kumpiga Jose Forero wa Panama. Bondia huyo atakuwa ni kibarua kigumu cha kutetea taji hilo mbelea ya KOOS SIPHO SIBIYA kutoka AFRIKA YA KUSINI

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi,Yusuph Singo alisema maandalizi ya pambano hili yalianza siku tarehe 5 August siku ya hafla ya kumpongeza bingwa huyo ambapo mgeni  alikuwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Harrison Mwakyembe ambapo Uongozi wa  bondia hiyo ilimwelezea Waziri mwenye dhamana na michezo kwamba, mkanda huo unapaswa kutetewa katika kipindi cha miezi mitatu tangu alipoupata na tayari kulikuwa na ofa mezani za kuutetea mkanda huo kutoka katika nchi za Marekani, Ujerumani na Ufilipino.
 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC, Matina Nkurlu (kushoto)akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani)  katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam,  wakati  wa kuwatambulisha  Bondia Mtanzania Ibrahim  Mgendera(Katikati) anayetarajia kutetea ubingwa wake wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight dhidi ya bondia kutoka Afrika ya Kusini KOOS SIPHO SIBIYA(hayupo pichani)  Pambano hilo la kimataifa la ngumi za kulipwa  limedhaminiwa na Vodacom Tanzania na Azam TV na  litafanyika  jumamosi  kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam,Kulia ni Mkuzaji wa Vipaji  vya ngumi Tanzania, Joe Anea.
 ondia Mtanzania,Ibrahim Mgendera(Kushoto)atakaye utetea ubingwa wake wa mkanda wa dunia wa Baraza la Ngumi Duniani (Global Boxing Council – GBC) uzito wa “Lightweight” (kushoto) na bondia kutoka nchini Afrika Kusini,KOOS SIPHO SIBIYA wakitambulishwa na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania PLC,Matina Nkurlu kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa mkutano na vyombo vya habari  uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, pambano hilo  la kimataifa la ngumi za kulipwa limedhaminiwa na Vodacom Tanzania,Azam TV litafanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akishuhudia mabondia Ibrahim Mgendera kutoka Tanzania na kocha wake (wapili kushoto)na bondia kutoka nchini Afrika Kusini,KOOS SIPHO SIBIYA na kocha wake(wapili kulia)wakitambulishwa kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa mkutano na waandishi hao uliofanyika Habari Maelezo jijini Dar es Salaam,  pambano hilo  la kimataifa la ngumi za kulipwa limedhaminiwa na Vodacom Tanzania PLC, AzamTV litafanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam,Katikati ni mwamuzi wa mpambano huo wa Kimataifa  kutoka nchini Ujerumani, Arno Pokrandt.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...