Mtoto wa marehemu Chacha Wangwe, Bob Wangwe, Wa kwanza kulia na Wakili wake Benedict Ishabakaki, mwenye suti ya bluu, wakitoka katika viunga vya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kufanikiwa kuruka kiunzi cha kwenda jela mwaka mmoja na nusu kwa kulipa faini ya sh. Milioni tano.
Pamoja na kulipa faini hiyo na kuwa huru wangwe amesema anatarajia kukata rufaa hivi karibuni kwani hajaridhika na uamuzi uliotolewa mahakamani hapo kwa sababu nyingi, Mojawapo ikiwa Hakimu hakusema kama ujumbe wake ule alioposti ulikuwa wa uchochezi au la.
Amesema, suala lolote la kutoa maoni siyo suala la mjadala, lipo kikatiba na ni haki ya watu wote ya msingi.
Mapema leo Novemba 15/2017 Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alimuhukumu Wangwe kulipa faini ya Sh.Milioni 5 ama kwenda jela mwaka mmoja na nusu baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kuchapisha taarifa ya uongo kwenye mtandao wa Facebook.
Katika kesi hiyo namba 167, Chacha Wange anatuhumiwa kwa kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.
Inadaiwa Machi 15/2016 alichapisha taarifa iliyosema,
) “….Tanzania ni ambayo inajaza chuki wananchi.… matokeo ya kubaka Demokrasia Zanzibar ni hatari zaidi ya Muungano wenyewe…. Haiwezekani nchi ya Zanzibar kuwa koloni la Tanzania Bara kwasababu za kijinga.”
Picha ya juu, Prof. Samwel Mwita Wangwe akishuka ngazi za mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kumaliza kulipa faini ya mtoto wake,Bob Wange aliyepatikana na hatia ya kuchapisha taarifa ya uongo kwenye mtandao kupitia ukurasa wake wa facebook.PICHA/HABARI NA KARAMA KENYUNKO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...