Na David John Misungwi
WANANCHI wa Kijiji cha Mwasonge kilichopo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza wameiomba Serikali kuharakisha ujenzi wa Daraja linalotenganisha wilaya hiyo na Wilaya ya Nyamagana.
Wamesema kuwa wananchi wa wilaya hizo hususani wanaoishi mpakani wamekuwa wamekuwa wakipata adha kubwa kutokana na serikali kushindwa kujenga Daraja.
Akizungumza Wilayani hapa leo Mwenyekiti wa Kijiji hicho cha Mwasonge Masumbuko Reuben alisema Tangu dunia iumbwe Serikali licha ya kutambua umuhimu wa eneo hilo lakini haijawahi kutengeneza Barabara hiyo wala Daraja.
"Naiomba sana Serikali yangu ifike mahala waone huruma dhidi ya wananchi hawa ambao wengi wao wanakatisha hapa kwenda Buhongwa katika wilaya ya Nyamaga kilometa mbili kuliko kuzunguka Usagala ambako ni zaidi ya kilometa 10."amesema Masumbuko.
Ameongeza kuwa eneo hilo linakuwa hatari zaidi linapojaaa maji kutokana na Mvua ambazo wakati mwingine zinanyesha mfululizo na kusababisha kutumia mitumbwi kuvusha wananchi hali inayohatarisha usalama.
Amefafanua kuwa miaka ya hivi karibuni kutokana na eneo hilo kujaa maji pameshawahi kutokea maafa ya raia hivyo kuna kilasababu na haja ya serikali kujenga Daraja katika eneo hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...