Wito umetolewa kwa wananchi kote nchini kuweza kujijengea utamaduni wa kuwekeza katika mfumo wa hisa na hasa katika hisa za Benki ya Maendeleo 

Wito huo kwa umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo, Ibrahim Mwangalaba jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kusogezwa mbele kwa zoezi lao la kuuza hisa za benki hiyo.Mwangalaba alisema njia kubwa ya kuwasaidia wananchi katika kujikwamua kimaisha ni kuchangamkiakia fursa zinazojitokeza ikiwemo ya kununua hisa za benki hiyo.Zoezi la uuzwaji wa hisa za benki hiyo ambalo lilianza Septemba 21, mwaka huu na lilikuwa limalizike leo sasa litandelea hadi Desemba 4, mwaka huu ili Watanzania wengi waweze kunufaika nalo.

Aliongeza kuwa lengo lao ni kuuza hisa zaidi ya mil.17 kwa Watanzania wapatao 170,000 kutoka mikoa yote ya Tanzania.Benki ya Maendeleo ni ya Watanzania wote, hivyo tumeona ni vema zoezi hilo lifanyike nchi nzima kwani awali tulikuwa tayari tumewafikia Watanzania kutoka mikoa 13 pekee na sasa tutatumia muda ulioongezwa kufika mikoa yote," alisema Mwangalaba.

Hisa moja inauzwa kuanzia sh.600 na kima cha chini cha kumiliki hisa ni 100.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...