Usajili Vitambulisho vya Taifa mkoani Singida umezidi kushika kasi wananchi wakifika kwa wingi kupata huduma ya Usajili unaohusisha uchukuaji wa alama za Kibiolojia, picha na Saini ya Kielektroniki.

Kwa kushirikiana kwa karibu na Maafisa Usajili, Watendaji wa Kata na Serikali za Mtaa, watumishi wa Mamlaka wamekuwa wafakifanya jitihada kubwa za kuhakikisha Wananchi wanatambua umuhimu wa kuwa na Vitambulisho vya Taifa pamoja na Matumizi yake Msingi na kushiriki kikamilifu kujisajili. 

Pamoja na misururu mirefu wananchi hao wameonyesha kutokata tamaa kwa foleni ndefu badala yake wamekuwa wakihamasishana kushiriki ili kila mmoja kupata haki yake msingi kusajiliwa.

Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa 12 ya Tanzania ambayo zoezi hilo linaendelea kwa sasa ukiwemo mkoa wa Mbeya, Njombe, Songwe, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita na Iringa.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA Ndugu Thomas William pamoja na Ndugu Innecent Baraza Meneja Usimamizi wa Majengo (Kushoto) wakifuatilia kwa karibu Uingizwaji wa taarifa za waombaji wa Vitambulisho vya Taifa wakati wa Zoezi la Usajili na Utambuzi linaloendelea Mkoa wa Singida. 
Wanachi katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida, wakifanyiwa usajili wa Maombi ya Vitambulisho vya Taifa katika zoezi la Usajili wa Mkupuo (Mass Registration) linaloendela hivi sasa Mkoani humo.
Baadhi ya Wananchi katika kata ya Kindai Halmashauri ya Manispaa Singida wakiwa kwenye foleni kuelekea kwenye chumba cha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki. 
Mkuu wa Kitengo cha Biashara Mamlaka ya Vitambulisho Ndugu Thomas William akisimamia zoezi la ugawaji wa fomu za Usajili wa Vitambulisho vya Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...