Na Bashir Yakub.

Yafaa kujua utaratibu unaotakiwa kufuatwa kabla ya kufutiwa hati miliki ya ardhi (nyumba/kiwanja). Unapojua utaratibu huu ndipo unapojua kama ulionewa au hapana. Na kuonewa ni pamoja na kukiuka utaratibu. Na kukiuka taratibu yoyote ya kisheria kunabatilisha mchakato wa kufutwa kwa hati yako na kutakiwa kurudishiwa eneo lako au fidia.

Makala yaliyopita tulieleza mambo ambayo ukifanya unahesabika kukiuka masharti ya umiliki wa ardhi na ni hapo unapoweza kufutiwa umiliki. Leo tuangalie utaratibu wa kufuta umiliki ikiwa imethibitika kuwa tayari umekiuka masharti hayo. Sheria namba 4 ya 1999 , Sheria Ya ardhi imeeleza utaratibu wa kufuta umiliki wa ardhi.

UTARATIBU.
1.Ni lazima uwe umekiuka masharti au moja ya masharti uliyopewa wakati unakabidhiwa ardhi/hati kwa mujibu wa kifungu cha 48 ( 1) cha Sheria ya ardhi. Usikubali kufutiwa umiliki ikiwa hujakiuka sharti/masharti ya umiliki uliyopewa, labda iwe vinginevyo.

2. Baada ya kuwa umekiuka masharti yafaa upewe taarifa maalum( notice) kwa mujibu wa kifungu 48(2). Ni taarifa inayoeleza masharti ya umiliki uliyokiuka na onyo la kufutiwa umiliki. Taarifa hiyo ni ya siku 90(miezi mitatu). Taarifa hiyo utapewa wewe mmiliki na kila mwenye maslahi katika ardhi hiyo mf, mpangaji, mrehani nk. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...