* WATALII KURUHUSIWA KWA KIBALI MAALUMU
Na Said Mwishehe,Blogu ya Jamii.
SERIKALI imepiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni ikiwamo ‘dola’ kuanzia Januari 1 mwaka 2018, na kueleza bei zote za huduma na bidhaa zitangazwe kwa Shilingi ya Tanzania.
Akizungumza Dar es Salaam leo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk.Philip Mpango wakati anaelezea mwenendo wa hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/2018.
Dk.Mpango kabla ya kutoa agizo hilo,amefafanua suala la matumizi ya fedha za kigeni sambamba na Shilingi ya Tanzania nchini linasimamiwa na Sheria ya Usimamizi wa fedha za kigeni ya mwaka 1992, sheria ya Benki Kuu ya Tanzania(BoT) ya mwaka 2006, na tamko la Serikali ya mwaka 2007 kuhusu matumizi ya fedha za kigeni kulipia bidhaa na huduma katika soko la ndani.
Amesema matumizi ya fedha za kigeni sambamba na Shilingi ya Tanzania wakati wa kufanya miamala mbalimbali yanaweza kuwa na athari kiuchumi ikiwa pamoja na kudhoofisha thamani ya shilingi.
“Sheria iliyopo kwa sasa haikatazi jambo hili bali inasisitiza sarafu ya Tanzania ndio fedha halali na mtu au taasisi yoyote itakayekataa kuupokea malipo ya shilingi yetu tutachukua hatua za kisheria.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Hali ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2017/18 ambapo alitoa agizo kwa vyombo vya ulinzi kuwakamata wanaowalazimisha watanzania kufanya malipo kwa Dola badala ya Shilingi, mkutano ulifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...