Kumekuwa
na taarifa mbalimbali, hamaki na kejeli zinazoenea katika mitandao ya kijamii
kuhusiana na taarifa iliyotolewa tarehe 27 Novemba 2017, Mnazi Mmoja kwenye uzinduzi
wa Mkakati wa Taifa wa Kondom kuhusu mpango wa Serikali kununua na kusambaza
kondom 500,000,000 katika kipindi cha miaka mitatu 2018 hadi 2020.
Tunapenda
kuukumbusha umma wa Watanzania kwamba maambukizi ya VVU na UKIMWI bado ni
tatizo katika nchi yetu. Takriban watu 1,400,000 wanakadiriwa kuwa na VVU. Hivyo
katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI Serikali inaendeleza afua mbalimbali ili kuzuia
maambukizi mapya.
Asilimia 40% ya maambukizi mapya yanatokea miongoni mwa vijana wenye umiri wa miaka 15-24. Aidha makundi maalum kama vile wanaojidunga madawa ya kulevya, wanaofanya biashara ya ngono na wale wanaoamiiana wa jinsia moja wako katika hatari kubwa ya kupata maambukizi. Makundi mengine ya walio katika hatari ni waendesha magari ya masafa marefu, wavuvi na wananchi wa kwenye migodi.
Asilimia 40% ya maambukizi mapya yanatokea miongoni mwa vijana wenye umiri wa miaka 15-24. Aidha makundi maalum kama vile wanaojidunga madawa ya kulevya, wanaofanya biashara ya ngono na wale wanaoamiiana wa jinsia moja wako katika hatari kubwa ya kupata maambukizi. Makundi mengine ya walio katika hatari ni waendesha magari ya masafa marefu, wavuvi na wananchi wa kwenye migodi.
Wizara
inatekeleza afua mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushauri nasaha na kupima uwepo
wa VVU, na kisha kuanza tiba na matunzo, pamoja na kutoa dawa za kufubaza kwa
watakao kuwa na maambuzi ya VVU. Kuna afua pia za kuzuia maambukizi ya mama
kwenda kwa mtoto, kutoa elimu ya VVU/UKIMWI na afya uzazi kwa vijana, elimu
kuhusu VVU/UKIMWI kwa jamii na tohara kwa wanaume.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...