Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh muhamed Utaly ametoa siku kumi na nne kwa wafugaji waliovamia maeneo yaliyotengwa kwaajili ya shughuli za kilimo katika kata ya Melela,kuondoka mara moja katika maeneo hayo na kupisha shughuli zilizo kusudiwa .

Tamko hilo la mkuu wa Wilaya linafuatia hivi karibuni baada ya ofisi yake kupokea barua ya malalamiko kutoka kwa wafugaji, wakiilalamikia serikali ya kijiji cha melela kuwa wamevamia katika eneo lao wanaloishi na sasa wanataka kuligawa kwa wakulima kwa shughuli za kilimo ,jambo ambalo lilimlazimu mkuu huyo wa Wilaya kwenda kukutana na pande hizo mbili ili kupata muafaka.

Awali akitoa maelezo kwa niaba ya serikali ya kijiji mwenyekiti wa kijiji hicho Said Membe amesema kuwa eneo hilo linalolalamikiwa na  wafugaji lilitengwa maalum  kwa shughuli za kilimo na kufuata taratibu zote za kisheria .

Bw membe amesema wao kama serikali ya kijiji wapo kwaajili ya kufuata na kusimamia taratibu za kisheria na kwakutambua hilo ofisi yake imeanzisha mchakato wa kukusanya maombi kutoka kwa wananchi wanaohitiji maeneo ya kulima na mchakato utakapo kamilika basi watayarudisha kwa wananchi wenyewe ilizoezi lakugawa mashamba hayo ufanyike kwa kufuata taratibu zote za kisheria.

Naye bwana wecha kwaniaba ya wafugaji waliopeleka malalamiko hayo kwa Mkuu wa Wilaya amethibitisha kuwa nikweli wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila kuwa na utamburisho rasmi  wa kisheria unaowapa uhalali wa kumiliki maeneo hayo ukiacha mfugaji mmoja ambaye ndiye anayetambulika kisheria na serikali ya kijiji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...