ZANZIBAR na Sharjah zimekubaliana kuendelea
kuimarisha uhusiano na ushirikiano wao uliopo katika kuimarisha sekta mbali
mbali za maendeleo zikiwemo elimu na biashara,
Katika mazungumzo
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Makaazi ya Mtukufu Dk. Sheikh Sultan Mohammed Al
Qasimi mjini Sharja, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein na kiongozi huyo wote kwa pamoja walisisitiza haja ya
kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo kwa lengo la kuimarisha sekta hizo
muhimu za maendeleo.
Rais Dk. Shein kwa upande
wake alimpongeza Dk. Sultan kwa hatua zake za kuendelea kuiunga mkono Zanzibar
katika kuimarisha miradi ya maendeleo ukiwemo mradi wa maji.
Pamoja na hayo, viongozi
hao walizungumza jinsi ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano katika kuimarisha
sekta ya elimu hasa ikizingatiwa kuwa Sharjah imeweza kupata mafanikio katika sekta hiyo kutokana
na kuwa na miundombinu mizuri ya elimu vikiwemo vyo vikuu.
Aidha, Dk. Shein
alieleza haja kwa Sharjah kutoa ushirikiano wake kwa Zanzibar katika sekta ya
elimu kupitia Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), jambo ambalo Dk. Sheikh
Sultan Mohammed Al Qasimi ameliunga mkono.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizunguma na Mtukufu Dk. Sheikh Sultan Bin Mohammed Al Qasimi alipofika katika makaazi yake kwa mazungumzo akiwa katika ziara yake katika Nchi za Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...