Kikao cha kamati ya Mashindano kilichokutana Desemba 29, 2017 kwenye makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kujadili mchezo namba 31 na 32 uliohusisha timu za Abajalo FC dhidi ya Tanzania Prisons ya Mbeya na ule kati ya Mvuvumwa na JKT Ruvu katika Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) iliyokuwa ifanyike Desemba 20, 2017 kwenye Uwanja wa Uhuru na Chamazi.


Kamati ilikaa na kupitia taarifa mbalimbali za michezo hiyo.

Kamati kupitia kanuni ya 24 kifungu cha (1) katika mchezo kati ya Abajalo FC na Tanzania Prisons imeipa ushindi timu ya Tanzania Prisons baada ya kubaini Abajalo kukiuka kanuni hiyo.

Kwenye mchezo mwingine kati ya Mvuvumwa na JKT Ruvu Kamati baada ya kupitia na kujiridhisha imeipa ushindi timu ya JKT Ruvu baada ya Mvuvumwa pia kukiuka kanuni ya 24 kifungu (1).

Kwa maamuzi hayo timu za Tanzania Prisons na JKT Ruvu zinafuzu kwenda kwenye hatua ya tatu(3) ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...