Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe akiwapongeza wajumbe wa kamati ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo kwa ubunifu waliyofanya katika siku ya uzinduzi uliyofanywa hivi karibuni na Makamu wa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan, katika Kikao cha Tathimini  ya Uzinduzi wa Kampeni hiyo  kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bi. Leah Kihimbi ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sanaa kutoka Wizara Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na kutoka kulia ni Mjumbe wa Kamati hiyo Bi.Shani Kitogo ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Lugha kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo Bi.Leah Kihimbi (kulia) ambaye ni Mkurugenzi  Msaidizi Idara ya Sanaa  kutoka Wizara Habari Utamaduni Sanaa na Michezo akieleza mafanikio ya uzinduzi wa kampeni hiyo kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) ikiwemo kupokea maombi kutoka taasisi mbalimbali kuomba wanakamati kwenda kutoa mafunzo kuhusu suala la uzalendo kwa watumishi wa ofisi zao,katika kikao cha tathimini ya uzinduzi wa Kampeni hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa Kamati ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo Bi.Joyce Fissoo ambaye ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini akitoa mapendekezo katika kikao cha tathimini ya uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam kuhusu Makala ya viongozi na wadau waliyozungumzia suala la uzalendo kwa taifa itakapo kamilika iweze kusambazwa nchini nzima katika Shule za Msingi na Sekondari kwa ajili ya kuwapa fursa watoto hao kujifunza kuhusu uzalendo.



Mjumbe wa Kamati ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uzalendo Bw.Mrisho Mpoto akitoa maoni ya mambo mbalimbali yanayoweza kufanikisha kampeni hiyo kuwa endelevu ikiwemo wajumbe kufanya tafiti kwa nchi zenye uzalendo kama China kwa lengo la kuhakikisha taifa linaelewa umuhimu wa uzalendo na manufaa yake katika kikao cha tathimini ya uzinduzi wa kampeni hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...