Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda , Leo amehaidi Kuijengea Nyumba ya Vyumba Vinnie (4) Familia ya Mwandishi (mpiga picha) wa Magazeti ya Serikali TSN wanaochapisha Magazeti ya Habari Leo na Daily News Marehemu Athumani Hamis ambae amezikwa Leo katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam. 

Ahadi hiyo Imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TSN Dkt. Yonaz kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda ambae aliombwa kuisadia familia ya Marehemu ambayo ina watoto Wanne wanaosoma uku wakiwa wanaishia kwenye Nyumba ya kupanga kutokana na Baba yao kuugua kwa zaidi ya Miaka 10 na hivyo kushindwa kufanya kazi. 

 Dkt. Yonaz amesema Mhe Makonda kwa kutambua mchango wa tasnia ya Habari hususani waandishi wa Habari amekubali kujenga Nyumba hiyo kama kielelezo cha Kumuenzi Marehemu Athumani ambae katika Uhai wake alikuwa Mpiga Picha Mahiri wa Magazeti ya Serikali nchini. 

 Hatua hii imepokelewa kwa Furaha na baadhi ya waandishi wa Habari ambao wamesema Kitendo cha Makonda kukubali Kuijengea Nyumba Familia ya Marehemu Athumani mbali na kuwafuta Machozi ya Huzuni, Bali kimekuwa ni fundisho Tosha kwa Baadhi ya waandishi ambao walikuwa Wakimchukia Mhe Paul Makonda pasipo sababu za Msingi, na kukifananisha Kitendo hiki na Ukamilifu wa Maandiko katika vitababu vitakatifu yanayotutaka TUWAPENDE ADUI ZETU.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda (katikati) akizungumza na Mhariri Mtendaji wa  Magazeti ya Serikali TSN Dkt. Jimmy Yonaz  kulia na Kaka wa Marehemu Athuman Hamis Dkt. Ibrahim Msengi nyumbani kwake Sinza Kijiweni jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...