Wananchi Mkoani Dodoma wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali katika Kujenga uchumi shirikishi unaogusa maisha ya wananchi baada ya Tanzania kutajwa na Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum) kuwa nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara kuwa na uchumi Jumuishi.
Akizungumza katika Mahojiano maalum mjini Dodoma Bibi Anyangwe Lupembe amesema ni jambo la kupongeza kwa hatua hiyo kwani haya ni matunda na juhudi kubwa zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kama ujenzi wa reli wa reli ya Kisasa (Standard Gauge) na Uzalishaji umeme.
Akifafanua Lupembe amesema kuwa kila mwananchi kwa sasa anaelewa kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuwahudumia wananchi wanyonge kwa kuhakikisha kuwa huduma muhimu zinapatikana kama Madawa, Elimu, miundo mbinu hali inayowapa fursa wananchi kushiriki katika shughuli za uchumi ikiwemo uzalishaji kutokana na mazingira wezeshi yaliyopo kwa sasa.
Aliongeza kuwa kasi ya ujenzi wa miundombinu kama barabara inawawezesha wananchi kushiriki katika uzalishaji na shughuli za maendeleo katika maeneo mbalimbali hapa nchi, hivyo uchumi kumilikiwa na wananchi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...