Na.WAMJW-DAR ES SALAAM
TANZANIA ni miongoni mwa nchi inayotumia dawa zilizo salama na ubora wa hali ya juu barani Afrika kutokana na udhibiti na umakini unaofanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini TFDA.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mamlaka wa Udhibiti na ubora wa dawa barani afrika unaofanyika jijini Dar es Salaam.
”Sisi kama Tanzania tunafanya vizuri sana katika udhibiti wa madawa yanayoingia,nataka niwathibitishie kwamba Tanzania dawa zetu tunazozitumia ni salama na zipo salama kwa uhakika mkubwa” alisema Dkt. Ndugulile .Aidha ,Dkt. Ndugulile alisema kuwa ongezeko la matumizi ya dawa ambayo hayana kiwango na kutumika katika mfumo wa tiba umeleta changamoto katika kuongeza gharama za matibabu nchini na barani Afrika
Kwa mujibu wa Dkt. Ndugulile amesema changamoto hizo zinasababisha wagonjwa wengi kukaa hospitalini,kuongeza gharama, kuathiri matokeo ya mgonjwa na hatimaye vifo pamoja na kuleta usugu wa dawa kwa kutumia dawa zisizo na kiwango .
TANZANIA ni miongoni mwa nchi inayotumia dawa zilizo salama na ubora wa hali ya juu barani Afrika kutokana na udhibiti na umakini unaofanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini TFDA.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mamlaka wa Udhibiti na ubora wa dawa barani afrika unaofanyika jijini Dar es Salaam.
”Sisi kama Tanzania tunafanya vizuri sana katika udhibiti wa madawa yanayoingia,nataka niwathibitishie kwamba Tanzania dawa zetu tunazozitumia ni salama na zipo salama kwa uhakika mkubwa” alisema Dkt. Ndugulile .Aidha ,Dkt. Ndugulile alisema kuwa ongezeko la matumizi ya dawa ambayo hayana kiwango na kutumika katika mfumo wa tiba umeleta changamoto katika kuongeza gharama za matibabu nchini na barani Afrika
Kwa mujibu wa Dkt. Ndugulile amesema changamoto hizo zinasababisha wagonjwa wengi kukaa hospitalini,kuongeza gharama, kuathiri matokeo ya mgonjwa na hatimaye vifo pamoja na kuleta usugu wa dawa kwa kutumia dawa zisizo na kiwango .
WaziriAfya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akiongea wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrika unaofanyika Jijini DaeEs Salaam na kuhudhuliwa na n chi zipatazo 17 za Afrika.
Dkt.Ndugulile akifuatilia mada (mwasilishaji hayupo pichani) katika mkutano huo
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.Agnes Kijo akiongea kwenye ufunguzi wa mkutano wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrika
Msimamizi wa kitengo cha Afya katika Shirika la Maendeleo ya Afrika (NEPAD) yenye makao makuu yake nchini Afrika ya Kusini Bi.Margareth Ndomondo akiongea wakati wa uzinduzi huo.Shirika hilo katika afya linasaidia kupunguza magonjwa yanayoikabili nchiza Afrika.
Dkt.Ndugulile akifuatilia mada (mwasilishaji hayupo pichani) katika mkutano huo
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.Agnes Kijo akiongea kwenye ufunguzi wa mkutano wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrika
Msimamizi wa kitengo cha Afya katika Shirika la Maendeleo ya Afrika (NEPAD) yenye makao makuu yake nchini Afrika ya Kusini Bi.Margareth Ndomondo akiongea wakati wa uzinduzi huo.Shirika hilo katika afya linasaidia kupunguza magonjwa yanayoikabili nchiza Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...