Na Agness Francis, Globu ya jamii 
Kikosi cha AzamFc kukutana na Mtibwa sugar robo fainali ya Michuano  Kombe la Shirikisho  la Azam Sports  Federation Cup (ASFC). 

Ambapo Mabingwa wa Afrika Mashariki na kati AzamFc watawakaribisha Mtibwa Sugar ya Mkoani Morogoro katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi

Akizungumza ofisini kwake leo Jijini Dar es salaam Ofisa Habari AzamFc Jaffary Maganga amesema kuwa wanasubiri tarehe ya mchezo huo  ambayo Bado haijatajwa. 

"Tunasubiri tu tarehe ya mchezo  ili kujua  mandalizi  yetu yanakwenda vipi na ukizingatia kikosi ni kigumu,  wana wachezaji wenye uwezo mkubwa  na Mwalimu  wao ni mzuri ila tutaakikisha tunalinda ushindi wa kuchezea  nyumbani ikiwa kila Timu Ina presha ya kutaka kusonga mbele zaidi ukizingatia ni mashindano ya mtoano ambapo ukifungwa unatolewa kwenye Michuano hiyo"amesema Jaffary.  

Maganga amemalizia  kuwa mashindano hayo yenye heshima kubwa  ambapo mshindi  wa michuano hiyo hupata nafasi ya kwenda kushiriki mashindano ya kimataifa  na kuiwakilisha Nchi.
Ofisa Habari Azam Fc, Jaffary Iddy Maganga akizungumza ofisini kwake leo Jijini Dar es salaam kuhusu mchezo wao dhidi ya Mtibwa sugar katika droo iliyochezeshwa ya robo Fainali ya mashindano ya kombe la shirikisho  Azam  sports federation cup   (ASFC).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...