Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze.
MADIWANI wa Halmashauri ya Chalinze, pamoja na mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete wamewasimamisha wakusanyaji wa ushuru kwenye baadhi ya vizuia, kutokana na kudaiwa kujihusisha na wizi na upotevu wa vifaa ili kupisha uchunguzi .
Pia, wameitaka halmashauri hiyo kutumia walinzi wenye silaha kwenye vizuia vikubwa vya ukusanyaji ushuru ikiwemo wa kokoto ili kukabiliana na wizi unaotokea mara kwa mara.
Maamuzi hayo ,yamefanyika baada ya madiwani hao kulalamikia wizi na hujuma zinazofanywa na wakusanyaji kwa kushirikiana na baadhi ya watendaji wa halmashauri wasio waaminifu.
Ridhiwani alisema ,kizuia cha Lugoba ni kero sanjali na Mpaji ,Mbwewe na Lunga ambapo kizuizi cha Lugoba kimeshavamiwa zaidi ya mara moja na matukio hayo yanaendelea kujitokeza hivyo wahusika lazima wachunguzwe.
“Mashine za ukusanyaji wa mapato zinaibiwa kirahisi rahisi ,hakuna kinachoendelea hivyo mchezo huu unavyoendelea halmashauri inapata hasara ”alifafanua Ridhiwani.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze Saidi Zikatim akuzungumza jambo wakati wa baraza la madiwani la Chalinze lililofanyika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Chalinze
Mbunge jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akuzungumza jambo wakati wa baraza la madiwani la Chalinze lililofanyika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Chalinze.
Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya Chalinze ,wakionekana pichani kusikiliza kwa makini jambo wakati wa baraza la madiwani.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...