Na  Bashir  Yakub.

Bubu yaani mtu asiyeweza kuongea  anaweza kuwa shahidi mahakamani iwapo ameshuhudia tukio. Kutokuwa na uwezo wa kuongea hakumwondolei sifa ya kushuhudisha kile ambacho amekishuhudia. 

Ikumbukwe ushuhuda unatokana na  na hatua ya mtu kuona, kusikia, kuhisi, kugusa, au  utambuzi wa tukio kwa namna yoyote  ambao umetokana na kiungo cha mshuhudiaji.

Yumkini, bubu wengi hawasikii. Na tumeona hapo juu kuwa ushuhuda ni pamoja na kusikia. Hata hivyo pamoja na kutosikia kwao bado wanavyo viungo vingine vya mwili ambavyo wanaweza kuvitumia kushuhudia tukio. Viungo hivyo ni pamoja na macho, mikono kugusa, ulimi kuhisi,akili katika utambuzi nk.


1.  SHERIA KUHUSU BUBU SHAHIDI.

Kifungu cha 128( 1 )  cha Sheria ya Ushahidi, Sura ya 6 kinasema kuwa  mtu ambaye  hawezi kuongea(bubu) anaweza kutoa  ushahidi wake  katika namna nyingine ambayo itaweza kuwa fanisi na ya kueleweka.  Njia fanisi na ya kueleweka ni kama kupitia maandishi/kuandika ikiwa anao uwezo wa kuandika, na kwa ishara ikiwa anao uwezo wa kutumia ishara.Wengi tunajua ishara kama njia kuu ya mawasiliano kwa bubu. Basi hiyohiyo inaweza kutumika kwa bubu kutoa ushahidi.

2.  HALI IKOJE KAMA HAKIMU/JAJI HAELEWI  ISHARA YA BUBU.

Bubu anapotoa ushahidi wake kwa ishara panatakiwa pawepo mtu ambaye atatafsiri ishara zile kwa maneno. Hata kamaHakimu/Jaji angekuwa na uwezo wa kujua ishara za bubu bado mtu anayetafsiri anatakiwa kuwepo. Hii ni kwasababu mahakamani hayupo hakimu tu. Bali wapo wapo wengine kama upande wa mashtaka , upande wa utetezi ambao wangependa kujua nini bubu anaongea katika ishara zake ili wapate kumuhoji na kumuuliza maswali kuhusu kile alichoongea.

                    KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...