Mkuu wa wilaya Temeke Felix Lyaniva
Walimu wa Madrassa waliohudhuria kikao hicho

Na Zainab Nyamka,Globu ya jamii
MKUU wa Wilaya ya Ilala Dar es Salaam Felix Lyaniva amewashauri waumini wa dini ya Kiislamu kuepuka migogoro na badala yake waimarishe umoja na udugu ili kudumisha amani iliyopo katika nchi yetu iendelee kudumu. 

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na walimu wa madrassa mbalimbali zilizopo wilayani Temeke jijini Dar es Salaam katika mkutano ulioandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania(Bakwata), Wilaya ya Temeke uliofanyika katika Chuo cha Ualimu (DUCE).

Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Da es Salaam Alhadi Mussa Salim amewataka waumini wa Kiislamu kufuata kauli mbiu ya baraza hilo inayosema "Walimu, tujitambue, tubadilike na tuache mazoea" na kufafanua ili kutengeneza jamii yenye maadili mema na uadilifu kwa jamii ya kiislamu na Mkoa kiujumla. 

Pia amewasisitiza walimu wa madrassa kuwafundisha wanafunzi wao yaliyo mema na kutengeneza mtaala mmoja wa kufundishia masomo ya dini ya kiislamu.Pamoja hayo wananchi wa Wilaya Temeke wanatakiwa kudumisha ulinzi na usalama wa wilaya yao."Kwani jamii yoyote yenye amani na utulivu ndio huchochea maendeleo ya familia na Taifa kwa ujumla,"amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...