Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk.Ashanti Kijaji amesema kuwa mamlaka ya Masoko na Mitaji ni injini katika maendeleo ya uchumi hivyo ni lazima mamlaka hiyo iwafikie wateja.

Kijaji aliyasema hayo wakati akitunuku vyeti kwa wahitimu wa mamlaka hiyo waliopata kwa kushirikiana na chuo cha Uingereza CISI katika fani ya masoko na mitaji, amesema kuwa watu hawana uelewa juu ya masoko na mitaji hivyo wanatakiwa kufikia wateja katika kutimiza adhima ya serikali ya awamu ya tano yenye Kauli mbiu ya nchi ya viwanda.

Amesema Mamlaka kwa kutumia watalaam hao lazima wafanye kazi katika kujenga nchi  na kutoa elimu  kuhusiana na masoko na mitaji.Amesema kuwa kampuni zipo nyingi lakini hazijaweza kuingia katika soko la hisa ni kutokana na kampuni hizo kushindwa kufikiwa ikiwa ni pamoja na kupata elimu.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa katika kufanya kazi mamlaka hiyo lazima iweke mpango mkakati katika kuhamasisha kampuni ziingie katika soko la hisa.Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo,Dk.John Mduma amesema kuwa wanaendelea katika kutoa huduma ikiwa ni pamoja kufanyia kazi maagizo ya Naibu Waziri katika kuwafikia wateja na kuleta matokeo chaya ya maendeleo ya uchumi.

Dk. Mduma amesema kuwa katika kuwa sasa watafungua dirisha la  uhamasishaji katika  kufikia kampuni ziweze kuingia katika soko la hisa.
Afisa Mtendaji Mkuu , Nicodemus Mkama amesema mkataba wa huduma kwa wateja waliouzindua watawafikia wateja wote kuingia dhamana ya masoko na mitaji katika kuendrleza miradi mbalimbali nchini.

 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashantu Kijaji, akizungumza mara baada ya kuwatunuku vyeti wahitimu wa kozi ya ushiriki katika Masoko ya mitaji na uzinduzi wa Mkataba wa huduma kwa Wateja.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa CMSA, Nicodemus Mkama akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi katika uzinduzi w akitabu cha huduma kwa wateja.

 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashantu Kijaji, akizindua kitabu cha Msaada wa huduma kwa wateja
 Mwenyekiti wa TSEBA,George Fumbuka akitoa neno la Shukrani kwa waziri mara baada ya kumaliza kuzinduliwa kwa kitabu cha Mkataba wa huduma kwa wateja.

  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashantu Kijaji, akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa wahitimu wa kozi ya ushiriki katika Masoko
 Baadhi ya Wadau walioshiriki katika uzinduzi wa kitabu cha huduma kwa wateja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...