Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, leo (Alhamisi) amekutana na kuwa na mazungumzo na  Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Gambia Mhe.   Hassan Bubacar Jallow.
Jaji Mkuu wa Gambia, yupo hapa  nchini kwa  ziara ya kikazi    ya kujifunza na kujipatia uzoefu kuhusu mfumo wa utoaji haki  hapa nchini pamoja na maboresho mbalimbali  yakiwamo ya maslahi ya  watumishi yanayoendelea katika   Mahakama ya Tanzania na Taasisi  nyingine za  Sheria na  utoaji  haki.
Jaji Mkuu  Jallow amemueleza Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dk. Adelardus Kilangi kwamba, Gambia, baada ya mabadiliko ya Serikali yaliyofanyika mwaka jana nchini humo, ipo katika mchakato wa kuifanyia  mabadiliko na maboresho   sekta ya sheria nchini humo.
"Nimekuja kwa ziara ya kikazi kwa madhumuni ya  kujifunza  kutoka Tanzania namna gani na sisi (Gambia) tutakavyoweza kuboresha na kuifanyia mageuzi makubwa  sekta  yetu ya Sheria na mfumo mzima wa  utoaji wa haki".
Akabainisha kwamba, anafahamu, namna gani  Mahakama ya Tanzania imeweza,  kwa kushirikiana na   Serikali na  Wadau wa  Maendeleleo  hususani Benki ya Dunia  kufanya  mageuzi  na maboresha makubwa  katika mfumo wa utoaji haki.
 Mwanasheria Mkuu  Dk. Adelardus Kilangi akisalimiana na  Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe  Wilbroad Slaa walipokutana nje ya Jengo   ambalo lina Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki . Mwanasheria Mkuu alikuwa akimsubiri kumpokea mgeni wake Jaji Mkuu wa Gambia Mhe.  Hassan Jallow ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali akimlaki Mgeni wake Jaji Mkuu wa Gambia  Mhe. Hassan Bubacar Jallow mara alipowasili kwa mazungumzo. Jaji Mkuu Jallow alisoma  sheria Chuo Kikuu cha  Dar es Salaam (1970-1973) na pia amewahi kuwa Mwendesha Mashtaka wa iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda
( ICTR) (2003-2015).
Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dk. Adelardus Kilangi akibadilishana mawazo na Jaji Mkuu wa Gambia Mhe. Hassan Bubacar Jallow, leo Ofisi kwa Mwanasheria Mkuu. Jaji Mkuu yupo hapa nchini kwa ziara ya kikazi yenye madhumuni ya kujifunza uboreshaji wa sekta ya  sheria na utoaji haki hapa nchini. Baadhi ya mambo waliyobadilishana mawazo ni pamoja  na uwezeshwaji kwa wanasheria  wa Serikali na watumishi wengine katika  sekta ya  sheria  kimaslahi na kimafunzo.
Habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...