Na Humphrey Shao, Globu ya jamii

Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Warace Karia amesema atasimamia suala la bima kwa wachezaji wanaoshhiriki katika ligi mbalimbali zinazo simamiwa na shiriki hilo hili kuweza kuwawezesha wachezaji kupata haki zao kwa haraka pindi wanapopata matatizo wakiwa michezo katika maisha yao ya Soka.

Karia amesema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mafunzo kwa viongozi wa vilabu mbalimbali nchini juu ya umuhimu wa bima yaliyoratibiwa na Tasisi ya ISDL kwa kushirikiana na kampuni ya Bima ya Aliance life Insurance ya hapa nchini Tanzania.

"lazima niwaambie ukweli hili suala la Bima mimi kwa sasa nitalifatilia kw aukaribu sana kwa kuhakikisha kuwa kila mchezaji aliyesajiliwa katika kalbu ya ligi kuu na shirikisho anapatiwa Bima ya maisha hili kuweza kupunguza matatizo yanayoweza kujitokeza pindi mchezaji wanapopata matatizo wakiwa uwanjani aua mara baada ya kumaliza mpira wake"amesema Karia.

amesema kuwa kwa sasa lawama nyingi zinatumwa kwa shirikisho la sokoa kuwa aliwahudumii wachezaji wa zamani lakini msingi wa jambo lenyewe kuondokana na lawama hizo ni kuhakikisha kuwa wachezaji hawa kila mmoja anapata Bima ya Maisha yake hili aweze kijikwamua pindi anapopata matatizo.

Karia pia alitumia fursa hiyo kutoa Salamu za rambirambi kwa msiba wa mwanamichezo mkongwe aliyekuwa anakipiga na klabu ya Simba Arthur Mambeta amefariki dunia siku ya jana Jumatano baada ya kusumbuliwa na maradhi ya saratani kwa muda mrefu.
 Rais wa Shirikisho la Soka nchini(TFF),Warace Karia akizungumza wakati wa uzinduzi wa Semina kwa vilabu mbalimbali vinavyoshiriki Michuano ya Shirikisho nchini.
 Mwenyekiti wa ISDL , Dr T.M Katunzi akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais wa Shirikisho la Soka nchini(TFF),Warace Karia  kuzindua Semina kwa ajili ya Vilabu mbalimbali hapa nchini.

Viongozi wa klabu mbalimbali nchini wakifatilia kwa makini hotuba ya Rais wa TFF katika Semina Maalum iliyoandaliwa na ISDL kwa kushirikiana na Aliance Life Insuarance.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...