Na Anitha Jonas – WHUSM
Serikali
imetoa pole kwa Taasisi ya Sanaa na
Utamaduni Bagamoyo kwa kumpoteza Mwalimu mahiri John Mponda aliyekuwa
balozi wa tasnia ya Sanaa nchini.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana
Shonza katika ibada ya kumuaga marehemu huyo iliyofanyika katika Chuo cha
TaSUBa Wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kumuaga kwani anatarajiwa kuzikwa kijiji
cha Mbalizi Mkoani Mbeya.
“Tunatambua
mchango wa Mwalimu John Mponda katika tansia ya sanaa nchini na kupitia
wanafunzi waliyopita katika mikono yake pamoja na vikundi vya vijana
alivyovianzisha ambavyo amekuwa akivifundisha kazi za sanaa, hakika tumempoteza
mtu makini,”alisema Mhe.Shonza.
Akiendelea
kuzungumza katika msiba huo Mheshimiwa Shonza
aliwasihi wasanii waliyopata mafunzo kutoka
kwa mwalimu huyo kuwa mabalozi kwa
wasanii wenzao na kuwashauri misingi iliyobora katika katika kukuza na
kuendeleza kazi za sanaa.
Kwa
upande wa Mkuu wa Chuo cha TaSUBa Dkt.Herbert Makoye alisema kuwa marehemu
mwalimu Mponda ameondoka katika kipindi walichokuwa wanamuhitaji sana kwani
kwasasa taasisi hiyo ipo katika maandalizi ya Tamasha la Utamaduni la Bagamoyo
ambalo nilakimataifa na hufanyika kila mwaka na yeye alikuwa mratibu na mpaka mauti yanamfika
alikuwa akiwa shughulikia maandalizi hayo.
“Kwa
hakika msiba huu ni pigo kwa taasisi yetu na mwalimu huyu alikuwa kiungo
miongoni mwetu na alifanya kazi yake kwa weledi na kujituma alikuwa ni mtu
aliyeipenda kazi yake ,’’alisema Dkt.Makoye.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.
Juliana Shonza akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Mkufunzi wa
Sanaa katika Chuo cha Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) marehemu Mwl. John
Mponda leo kabla ya ibada ya kumuaga kwa
ajili ya safari ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika Mbalizi mjini Mbeya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...