Na Veronica Simba – Ngara
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema kuwa Serikali itaboresha mazingira ya uwekezaji wa Madini ya Nickel yanayopatikana Ngara mkoani Kagera lakini pia itahakikisha wawekezaji wanayaongezea thamani Madini hayo hapa nchini kabla ya kuyasafirisha nje ya nchi ili kuleta tija zaidi.
Aliyasema hayo jana, Machi Mosi alipotembelea Mradi wa Uwekezaji wa Madini ya Nickel wa Kabanga, uliopo wilayani Ngara, Mkoa wa Kagera, akiwa katika ziara ya kazi.
“Sisi kama Serikali tutahakikisha tunawaletea wawekezaji miundombinu ya Barabara, Reli na Umeme ili kuwajengea mazingira rafiki ya uzalishaji lakini kwa upande wao tunataka kuona uwekezaji makini; wachimbe na kuongeza thamani ya madini hayo hapa nchini. Badala ya kutoa Nickel kama malighafi, watoe bidhaa zinazotokana na Nickel.”
Alisema kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha Madini hayo muhimu, ambayo kwa sasa Soko lake Duniani limeanza kupanda, yanalinufaisha Taifa kwa kiwango kinachostahili.
Akifafanua, Naibu Waziri alisema kuwa, Nickel ikiongezewa thamani hapa nchini, miundombinu ya Reli, Umeme na Barabara ikaboreshwa; kutakuwa na uhakika wa kuuza Madini hayo kwa bei nzuri na kuleta ushindani kwenye Soko la Dunia.
Meneja Mkazi wa Mradi wa Kabanga Nickel, Andrew Msola akiwasilisha Taarifa ya Utendaji kazi wa Mradi huo kwa Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo na Ujumbe aliofuatana nao, alipotembelea na kukagua Mradi huo akiwa katika ziara ya kazi, Machi Mosi mwaka huu.
Sehemu ya shehena ya Madini ya Nickel kama ilivyokutwa wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo (hayupo pichani), katika Mradi wa Kabanga Nickel, Wilayani Ngara Mkoa wa Kagera, Machi Mosi mwaka huu.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kukagua Mradi wa Kabanga Nickel uliopo Wilayani Ngara, Mkoa wa Kagera, Machi Mosi mwaka huu akiwa katika ziara ya kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...