Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka alipomtembelea ofisini kwake kupata taarifa ya Viwanda na uwekezaji katika mkoa huo, tarehe 1 Machi, 2018.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri walipofika ofisi za SIDO Mkoa wa Njombe kuona utendaji wake.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akikagua eneo litakalojengwa majengo makubwa kwa ajili ya wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo, Mkoani Njombe tarehe 1 Machi, 2018.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage, akimsikiliza meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Njombe kuhusu utaratibu wanaotumia katika kupima mizigo ya wakulima na wafanyabiashara mkoani Njombe.
 Muonekano wa Kiwanda cha kuchakata Chai cha Unilever kilichopo mkoani Njombe ambacho kipo katika hatua za mwisho kukamilika kwa ujenzi wake.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza wakati wa mkutano na wafanyabiashara kujadili changamoto zianazowakabili wafanyabiashara katika mkoa wa Njombe Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri. 
Wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe waliokusanyika kumsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Hayupo pichani) na baadae kuuliza maswali kutokana na changamoto wanazokutana nazo na kupatiwa majibu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...