Na Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

OFISI ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kitengo cha ardhi , imemtaka Msajiri wa Hati wa Wizara ya Ardhu,Nyumba na Maendeleo ya Makazi kufuta mara moja hati namba 105525 wa Kiwanja namba 1003 kilichopo Mtaa wa Sekenke Kinondoni, chenye mgogoro uliodumu kwa miaka 10.

Kiwanja hicho kilikuwa kinagombewa na wananchi wawili ambao ni Ally Abdi na Seleman Marashed kutokana na familia kukiuza mara mbili huku pia kikiwa na namba mbili ambazo ni 212 na 1003.Ofisi hiyo imebaini kunaupindishaji mkubwa wa taratibu za uuzwaji na upimaji wa kiwanja hicho ambacho kilikuwa ni mali ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Kwa mujibu wa barua ya Ofisi ya mkuu wa mkoa kwenda Wizara ya Ardhi, iliyosainiwa na Ofisa Ardhi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Edgar Msolla, ya Februari 15 mwaka huu, baada ya uchunguzi mzito kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni ilibaini kuwepo ukiukwaji wa sheria.Uchunguzi huo umekuja baada ya Abdi kuwasilisha malalamiko katika ofisi hiyo kuhusu kiwanja hicho namba 212 ambacho kipo kwenye mchoro wenye Survey Plan D1.503/23 wa mwaka 1994.

Kiwanja hicho kina ofa iliyotolewa Aprili 18 mwaka 1964 kwa NHC ambao walikiuza kwa Moshi Majungu akiwa msimamizi wa mirathi ya baba yake Kondo Majenga.Abdi anadaiwa kununua kiwanja hicho mwaka 2004 kutoka kwa Moshi Kondo Majenga kwa niaba ya familia ya Kondo Majengo.Hata hivyo baada ya taratribu za mauziano hayo taratibu za kuhamisha miliki hazikukamilika.Imedaiwa kwa mara ya pili kiwanja hicho kiluzwa kwa tena na Moshi Mussa Majenga aliyeuwa msimamizi wa mirathi ya Kondo Majenga kwa Marshed mwaka 2008.
 Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Kinondoni Mjini,Mussa Embe akizungumza na waandishi wa habari nakufafanua kwamba mtaa wake unanyumba unanamba za nyumba nyumba 490 tu.
Ally Abdi akinonesha nyaraka mbalimbali za nyumba hiyo aliyo. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...