Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) katika hatua zake za  kutaka kuimarisha mtaji wake na kufanya kazi zake kwa ufanisi imewataka wateja wake 7,065 wenye mikopo sugu yenye thamani Tsh. bilioni 7.9, kulipa mikopo hiyo ndani ya siku saba vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo, Bi. Beng’i Issa alisema benki imeanza kuchukua hatua za kuimarisha mtaji wake kwa kuwataka wateja wake wenye madeni sugu kulipa madeni yao ndani ya siku hizo vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa. 

“Moja ya mambo yanayokwamisha  kuimarika kwa mtaji na kupanua huduma za kibenki ni kuwepo kwa mikopo sugu,” sasa tunawataka wateja wetu wenye mikopo sugu kulipa bila shuruti vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa, aliongeza kusema,Bi Issa ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Alisema hatua hiyo imechukuliwa ili kuhakikisha mtaji wa benki unaimrika na itasaidia kutoa huduma za kibenki kwa ufanisi. Wakopaji wengi wamepitiliza siku 90 za urejeshaji madeni ya mikopo yao na hiyo kinyume na utaratibu wa mikataba waliyokubaliana na benki wakati wanakopa.
Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya Wanawake (TWB), Bi. Beng’i Issa akisisitiza jambo wakati alipokuwa akitoa taarifa kwa vyombo vya habari juu ya benki hiyo ilivyojipanga kuimarisha mtaji wake kwa kuwataka wateja wake wenye madeni sugu kulipa madeni yao ya mikopo, wa pili kulia ni Mjumbe wa Bodi hiyo, Bw. Oswald Mutaitina, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Japhet Justine na wa pili kushoto ni Mjumbe wa Bodi hiyo Bw. Ramadhani Saidi. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...