Vee Money App katika kilele cha maendeleo ya mziki Afrika na dunia nzima
Vanessa Mdee anaungana na mastaa maarufu duniani ambao wanamiliki ‘majukwaa ya mtandaoni’ ya kuwasiliana na mashabiki wao
Je unafahamu kitu gani kinachowafananisha Taylor Swift, Ciara, na Vanessa Mdee? Naam, pamoja na kwamba wote ni wasanii wenye sauti nzuri na vipaji vikubwa, wote watatu wanamiliki majukwaa ‘app’ za kuwasiliana na mashabiki wao mtandaoni.
Hii ni njia mpya inayotumiwa na wasanii wakubwa ambao wana mashabiki wengi katika mitandao ya kijamii kama Facebook na Instagram, ukweli ni kwamba pamoja na mitandao hiyo mikubwa ya kijamii kutengeneza mabilioni ya dola kila mwaka wasanii hawapati mapato ya moja kwa moja kutokana na biashara hiyo.
Sababu nyingine kubwa ambayo inawafanya wasanii kama Kim Kardashian kuwa na majukwaa yao mtandaoni ‘app’ ni kwa sababu hawamiliki mashabiki wao wa mtandaoni ila mitandao ya kijamii ndiyo ina haki juu ya watu wanaoitumia, hii inamaanisha msanii mkubwa akifungiwa akaunti yake ya Facebook au Instagram anaweza kukosa njia ya kuwasiliana na mashabiki wake (Rob Kardashian ni mfano halisi).
Pamoja na ukweli kwamba majukwaa‘app’ pia zinaruhusu wasanii maarufu kuuza bidhaa mbalimbali na tiketi kwenye simu za mkononi lakini cha muhimu zaidi, inasaidia wasanii kufaidika kutokana na makampuni makubwa kutangaza kupitia majukwaa yao.
Vanessa Mdee anaungana na mastaa maarufu duniani ambao wanamiliki ‘majukwaa ya mtandaoni’ ya kuwasiliana na mashabiki wao
Je unafahamu kitu gani kinachowafananisha Taylor Swift, Ciara, na Vanessa Mdee? Naam, pamoja na kwamba wote ni wasanii wenye sauti nzuri na vipaji vikubwa, wote watatu wanamiliki majukwaa ‘app’ za kuwasiliana na mashabiki wao mtandaoni.
Hii ni njia mpya inayotumiwa na wasanii wakubwa ambao wana mashabiki wengi katika mitandao ya kijamii kama Facebook na Instagram, ukweli ni kwamba pamoja na mitandao hiyo mikubwa ya kijamii kutengeneza mabilioni ya dola kila mwaka wasanii hawapati mapato ya moja kwa moja kutokana na biashara hiyo.
Sababu nyingine kubwa ambayo inawafanya wasanii kama Kim Kardashian kuwa na majukwaa yao mtandaoni ‘app’ ni kwa sababu hawamiliki mashabiki wao wa mtandaoni ila mitandao ya kijamii ndiyo ina haki juu ya watu wanaoitumia, hii inamaanisha msanii mkubwa akifungiwa akaunti yake ya Facebook au Instagram anaweza kukosa njia ya kuwasiliana na mashabiki wake (Rob Kardashian ni mfano halisi).
Pamoja na ukweli kwamba majukwaa‘app’ pia zinaruhusu wasanii maarufu kuuza bidhaa mbalimbali na tiketi kwenye simu za mkononi lakini cha muhimu zaidi, inasaidia wasanii kufaidika kutokana na makampuni makubwa kutangaza kupitia majukwaa yao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...