Aliye kuwa Waziri wa Mambo ya Nje nchini Marekani Tillerson Rex.

Na Ripota Wetu
RAIS  wa Marekani Donald Trump amemfuta kazi Waziri wa Mambo ya Nje nchini humo Tillerson Rex na nafasi yake kuchukuliwa na Mike Pompeo.

Kupitia ukurasa wake wake Twitter Trump amesema Waziri Mteule wa Mambo ya Nje atafanya kazi nzuri na Tillerson hajui sababu ya yeye kuondolewa katika nafasi hiyo licha ya vyombo mbalimbali kuripoti kuwa ni sababu binafsi baina yake na Rais huyo.

Ikumbukwe tangu Trump aingie madarakani viongozi wengi wameachia ngazi zao wakiwemo washauri na viongozi wa masuala ya ulinzi na usalama katika ikulu ya marekani.

Waziri mteule Mike pompeo kabla ya uteuzi huu alikua Mkurugenzi wa Shirika la ujasusi nchini Marekani na ifahamike kwamba uteuzi huu umekuja katika kipindi cha maandalizi ya mkutano baina ya Donald Trump na Rais wa korea kaskazini Kim Jong Un aliyeomba kukutana na Trump mapema Mei mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...