Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
ALIYEKUWA  Rais   wa Brazil  Luiz Inancio Lula da Silva maarufu kama Lula ametakiwa kuanza kutumikia kifungo chake cha miaka 12 gerezani kwa tuhuma za rushwa ya Euro laki saba na tisini wakati wa utawala wake.

Licha ya Lula kukanusha madai hayo nusu ya majaji waliunga mkono kifungo cha da Silva licha ya wananchi wengi kutegemea mkongwe huyu wa siasa kuekana katika mbio za uchaguzi mkuu utakaofanyika mapema Octoba.

Lula anaungwa mkono na wafuasi  wake katika miji ya Sao na Bernardo ambao waliandamana kupinga adhabu hii na kutaka aachiwe huru.

Luiz Inancio da silva (72) alizaliwa October 27, 1945 akiwa Rais wa 35 kuiongoza Brazil kuanzia Januari 1 2003 hadi Januari 1 2011 na ikumbukwe kuwa Lula alikuwa rafiki wa karibu wa aliyekuwa kiongozi wa Cuba  Fidel Castro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...