Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta pamoja na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la madarasa kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji maalum katika Shule ya Msingi Msasani, Dar es Salaam, Aprili 6, 2018. Msada huo ni ya sehemu ya Benki ya CRDB katika kuisaidia jamii. Ambapo Benki hiyo imejiwekea sera maalum ya kusaidia jamii ambayo inalenga kurudisha kiasi cha asilimia moja ya faida ya Benki hiyo kila mwaka, ili ziende katika shughuli za kijamii, hususani katika nyanja za elimu, afya na mazingira.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akizungumza na kutoa pongezi kwa Benki ya CRDB ambapo aliishukuru benki hiyo kwa msaada huo wa madarasa na madawati kwa shule ya msingi Msasani. katikati ni Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa na kulia ni Mwalimu Edward Molel.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, pamoja na wanafunzi wenye uhitaji maalum, wakimsikiliza mmoja wanalimu wa shule hiyo alipokuwa akieleza jambo kwa lugha ya alama.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akimshukuru Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa kwa msaada huo waliotoa.
Picha ua pamoja na baadhi ya wanafunzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...