KAMANDA
wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa ameeleza
namna ambavyo wamemkamata na kumhoji msanii maarufu Nassib Abdul a.k.a
Diamond na kisha kumuachia kwa dhamana.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na Michuzi blog,Kamanda Mambosasa amesema alimakata Diamond jana kati ya saa 11 na saa 12 jioni na kisha walimhoji kutokana na kusambaza picha za utupu katika mtandao.
"Polisi tumemshikilia Diamond na kisha tukamhoji kwa kusambaza picha za utupu mtandaoni,"amesema Mambosasa na kuongeza kuwa hilo ni kosa la kimtandao hivyo sheria itachukua mkondo wake.
Alipoulizwa kama Diamond bado anashikiliwa Polisi au laa, Mambosasa amejibu baada ya kumhoji walimuachia kwa dhamana wakati upelelezi ukiendelea."Upelelezi ukikamilika tutaendelea na hatua nyingine za kisheria,"amesisitiza.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na Michuzi blog,Kamanda Mambosasa amesema alimakata Diamond jana kati ya saa 11 na saa 12 jioni na kisha walimhoji kutokana na kusambaza picha za utupu katika mtandao.
"Polisi tumemshikilia Diamond na kisha tukamhoji kwa kusambaza picha za utupu mtandaoni,"amesema Mambosasa na kuongeza kuwa hilo ni kosa la kimtandao hivyo sheria itachukua mkondo wake.
Alipoulizwa kama Diamond bado anashikiliwa Polisi au laa, Mambosasa amejibu baada ya kumhoji walimuachia kwa dhamana wakati upelelezi ukiendelea."Upelelezi ukikamilika tutaendelea na hatua nyingine za kisheria,"amesisitiza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...