KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa ameeleza  namna ambavyo wamemkamata na kumhoji msanii maarufu Nassib Abdul a.k.a Diamond  na kisha kumuachia kwa dhamana.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na Michuzi blog,Kamanda Mambosasa amesema alimakata Diamond jana kati ya saa 11 na saa 12 jioni na kisha walimhoji kutokana na kusambaza picha za utupu katika mtandao.

"Polisi tumemshikilia Diamond na kisha tukamhoji kwa kusambaza picha za utupu mtandaoni,"amesema Mambosasa na kuongeza kuwa hilo ni kosa la kimtandao hivyo sheria itachukua mkondo wake.

Alipoulizwa kama Diamond bado anashikiliwa Polisi au laa, Mambosasa amejibu baada ya kumhoji walimuachia kwa dhamana wakati upelelezi ukiendelea."Upelelezi ukikamilika tutaendelea na hatua nyingine za kisheria,"amesisitiza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...