
Mchezo huo wa aina yake utachezwa leo saa 10 jioni katika dimba la Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.
Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na Ofisa Habari Ofisi ya Meya wa Jiji la Dar es Salaam Christina Mwagala Meya huyo atakuwa miongoni mwa watazamaji wa mtanange huo mkali.
Kwa kawaida mechi ya Simba na Yanga huwa na watazamaji wengi wakiwemo viongozi mbalimbali wa Serikali na Wabunge,Ifahamike kuwa Mwita ni miongoni mwa maelfu ya mashabiki wa mpira wa miguu .
Katika mchezo huo Simba wanaingia uwanjani wakiwa wanaongoza ligi baada ya kujikusanyia pointi 59 ikicheza michezo 25 wakati Yanga wana pointi 48 wakiwa nafasi ya pili baada ya kucheza michezo 23.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...