Na John Mapepele, Dodoma 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewataka wawekezaji wa viwanda vya kuchinja Punda nchini kupandisha bei ya kununua wanyama hao badala ya shilingi laki mbili ya sasa kwa punda mmoja ili kudhibiti utoroshaji wa mifugo nje ya nchi ambapo inakadiriwa kuwa zaidi ya mifugo elfu kumi inatoroshwa mipakani kwa siku kwenda nje ya nchi inakonunuliwa kwa bei ya juu. 

Akizungumza leo baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika Kiwanda cha Punda cha Hua Cheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma alichokifungua hivi karibuni, Waziri Mpina alisema bei hiyo haiendani na gharama halisi ya ufugaji wa Punda hali inayowafanya wafugaji kuwatorosha mifugo na kulikosesha taifa mapato makubwa. 

Alisema ili punda aweze kufikia hatua ya kuchinjwa inachukua kiasi cha miaka miwili ambapo gharama zake za ufugaji zinakuwa juu ukilinganisha na bei ya shilingi laki mbili anayouzwa kwa wenye viwanda vya punda nchini.

Aidha alisema kumekuwa na utoroshaji mkubwa wa mifugo wanaokadiriwa kufikia takribani 1,614,035 kwa mwaka unaofanyika kwenye mipaka ya nchi yetu ambapo takribani shilingi bilioni 32.28 zinapotea kama ushuru na takribani shilingi bilioni 24.21 zinapotea kutokana na kodi ya mapato ambayo ingelipwa kwa nyama ambayo ingeuzwa hapo nchini. 

Aidha Mpina ameunda tume ya wataalam kutoka Wizarani kwa ajili ya kuja kufanya tathmini kama kiwanda hicho kimetimiza masharti yote yaliyotolewa na Serikali baada ya kukifungua Februari mosi mwaka huu ambapo alisema ikibainika kuwa kiwanda hakijakidhi masharti yaliyotolewa na Serikali kitachukuliwa hatua kali zaidi za kisheria ikiwa ni pamoja na kukifungia kufanya kazi zake. 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye miwani) akikagua kiwanda cha kuchinja Punda cha Hua Cheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma alichokifungua hivi karibuni leo. (Picha na Jumanne Mnyau) 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye miwani) akipokea maelezo ya usindikaji wa nyama Punda kutoka kwa mfanyakazi wa wa kiwanda cha kuchinja Punda cha Hua Cheng Limited Elizabeth Peter.(Picha na Jumanne Mnyau) 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(mwenye miwani) akitembezwa katika kiwanda cha kuchinja Punda cha Hua Cheng Limited kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma alichokifungua hivi karibuni na Meneja Mkuu wa kiwanda hicho bwana Xun Long Go .(Picha na Jumanne Mnyau) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...