Na Sixmund J. Begashe
Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA) Bw Adrian Nyangamale ameungana na wasanii wote, wapenda sanaa, Serikali ya Tanzani, na watanzania wote katika kuomboleza kifo cha aliewahi kuwa Kahimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni nchini Bi Joyce Hagu. 
“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa msiba wa Dada Joyce Hagu, ni juzi tu tulikuwanae Magomeni kwenye msafara wa Mh Waziri Dr Harison Mwakyembe alipotembelea wanamuziki wa zamani, tukitaniana na kucheka kama ilivyokuwa desturi yake, kumbe ndio alikuja kutuaga.’’ Aliandika Bw Nyangamale kwenye kundi la whatsap la shirikisho hilo lijulikanalo kama JAMVI. 

Kupitia ukurasa huo maarufu nchini wa JAMVI Bw Nyangamale aliongeza kuwa   Marehemu Joyce Hagu alikuwa msaada mkubwa kwenye tasnia ya sanaa za Ufundi nchini kwa kutumia taaluma yake ya sanaa kuuwashauri wasani mambo muhimu katika Sanaa na Utamaduni wa Mtanzania, kukosa na kutoa njia bora ya kujisahihisha pale wasanii wanapo kwende kinyume na maadili ya Utamaduni wa Mtanzania.

“Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA) tunatoa pole kwa Mhe Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, watumishi na wafanyakazi wa Wizara, na Taasisi zake, Mashirikisho ya Sanaa, Vyama, Vikundi na Jamii yote ya wasanii nchini. Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote bila kusahau Wanajamvi kwa msiba huu mzito.” Alimalizia Bw Nyangamale

Wakiungana na Rais wa TAFCA, wanajamvi Lilian Nabora, Mussa Sango, Wilhadi Tairo na Namsikiliza Mungu wameeleza kwa masikitiko makubwa namna walivyo pokea taarifa za msiba huo na kuwa Marehemu amefariki wataki ikiwa bado machango wake ulikuwa ukihitajika sana katika tasnia ya Sanaa na Utamaduni nchini, na kuahidi kuwa wataendelea kumkumbuka daima.

Taarifa za kuaga dunia kwa Msanii Msomi na Mwalimu gwiji wa sanaa nchini Bi Joyce Hugu zimedhibitishwa na kaka yake aitwae Gabriel pale alipo ongea kwa simu na mwandishi wa habari hizi akisema kuwa dada yao amekutwa na umauti akiwa amelala usiku wakumakia jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...