Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii
HATIMAYE yametimia, Droo ya Nusu Fainali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya imemalizika kupangwa mchana huu, kwa miamba ya soka barani humo kukutana uso kwa uso.
Real Madrid kutoka nchini Hispania itakuwa na kibarua cha kumenyana na Bayern Munich wakati Liverpool wao wakivaana na AS Roma.
Mkondo wa kwanza wa michezo hiyo inatarajiwa kupigwa kati ya April 24/25 wakati mkondo wa pili unatazamiwa kupigwa kati ya May 1/2mwaka huu.
Wakati huo huo Michuano ya UEFA Europa League, droo yake ya Nusu Fainali imemalizika mchana huu, kwa Arsenal ya Uingereza kuikabili Atletico Madrid ya Hispania na Olimpique de Marseille ya Ufaransa kuchuana na FC Salzburg.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...