Na Agness Francis,Blogu ya Jamii

MECHI ya wana Paluhengo Lipuli na vinara wa Ligi Simba uliotarajiwa kuchezwa  Ijumaa Aprili  20 mwaka huu katika Uwanja wa Samora Mjini Iringa imesogezwa mbele.

Mchezo huo wenye namba 202 wa Ligi Kuu ya Vodacom Lipuli dhidi ya  Simba SC  sasa hautachezwa kama tarehe ya mwanzo iliyopangwa na  (TFF).Umesogezwa  mbele kwa siku moja.

Bodi ya Ligi ya Mpira wa miguu Tanzania (TFF) wameamua Mechi hiyo ichezwe Aprili 21,mwaka huu kwenye uwanja huo huo wa Kumbukumbu ya Samora mkoani  Iringa.

Ambapo Sababu za mabadiliko hayo ni wamiliki wa uwanja kuutumia Aprili 20, 2018 kwa shughuli nyingine za kijamii.

Ikiwa  kwa mujibu wa ratiba Mbeya City inasubiri kuvaana na  Yanga SC Aprili 22  mara baada ya kurejea.

Kikosi hicho ambacho kipo  nchini Ethiopia kuchuana na  Welaita Dicha Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Mtanange huo utakaopigwa katika Dimba la Uwanja wa Sokoine uliopo Jijini Mbeya huku Mbeya city wakiwa wenyeji wa Yanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...