Na Leah Mushi( Afrika Kusini)

“Embu jiulize ni namna gani shujaa wa taifa angejisikia pale ambapo amekaa mbele ya watu wa rika tofauti jinsia tofauti wenye mirengo tofauti ya kisiasa wote wakimsifia na kumshukuru kwa werevu wake wakulipigania taifa?”

Maneno ya Mama Graca Machel mwanaharakati wa masuala ya wanawake na watoto wa Afrika akiongea mbele ya umati wa watu kutoka maeneo mbalimbali duniani waliofika kutoa salamu za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Winnie Mandela aliyefariki tarehe 2 Aprili 2018 nchini afrika kusini.

Winnie Madikizela-Mandela (81) alikuwa mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo hali iliyopelekea kufungwa mara kadhaa mbali na kuendelea kupokea vitisho lakini aliendea kuwa mwanaharakati mpaka mauti yaliyomfika. 

Winnie Mandela ambaye kwa wengi anafahamika kama mama wa taifa la Afika Kusini pia alikuwa mke wa Nelson Mandela  kwa miaka 38 toka mwaka 1958 mpaka walipoachana mwaka 1996 na kufanikiwa kupata watoto wawili.

Akiongea katika Msiba huo mama Graca Machel ambaye amekuwa akimuita Marehemu Winnie Mandela “dada mkubwa” amesema ni wakati sasa wa kuwaita mashujaa wa taifa na kuwashukuru wangali wakiwa hai kwakuwa hakuna ajuae kama wanasikia na kuona vile wanavyosifiwa wakati wa Misiba yao.

Pia amekemea tabia ya jamii kuwananga na kuwasema watoto wa wapigania uhuru kwakuwa wengi wao wamekosa miongozi na malezi bora ya wazazi kwakuwa wazazi wao walikuwa na ujasiri wa kuacha familia zao na kupigania taifa hivyo si sawa kuwasema na kuwanyooshea vidole badala yake waoneshe upendo zaidi kwao katika kile kilichofanywa na wazazi wao.

Kuhusu rambirambi na ahadi zinazotolewa misibani Mama Graca amewataka wananchi na wanasiasa kuacha maneno ya hadaa kwakuwa mengi yanayoahidiwa hayatekelezwi.

Akitolea mfano wa ahadi zilizotolewa wakati wa wa msiba wa Nelson Mandela miaka mitano iliyopita amesema “ kwasasa ukiangalia Afrika kusini mambo yamekuwa mabaya zaidi ya kipindi Mandela yuhai na hii inaonesha kiasi gani watu hawaishi ahadi zao walizoahidi na ndio jambo hata leo watu wengi wameahidi kuendeleza harakati za Winnie Mandela lakini nani anajua kama zitatekelezwa?”

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...