Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana akiwakaribisha wageni waalikwa katika ufunguzi wa siku ya Tanzania ambayo huadhimishwa tarehe 26 Aprili siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hafla ya maadhimisho hayo ilifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta Jijini Nairobi, Kenya. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Ababu Namwamba ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar akihutubia wageni waalikwa waliohudhuria katika mchaparo ulioandaliwa na ubalozi wa Tanzania nchini Kenya tarehe 26 April 2018. 
Viongozi wa Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jamhuri ya Kenya na Mkuu wa Mabalozi nchini Kenya wakikata keki katika kusheherekea maadhimisho ya muungano huo. 
Viongozi wa Serikali kutoka Kenya na Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa hafla hiyo, kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya, Balozi Macharia Kamau, Naibu Waziri Viwanda na Biashara, Mhe. Hassan Hafidh, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje, Mhe. Ababu Namwamba na Balozi mteule wa Jamhuri ya Kenya nchini Tanzania, Mhe. Kazungu Kambi. 
Viongozi pamoja na wageni waalikwa wakisherehekea kwa pamoja muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...