MKUU
wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema amewapongeza kazi
kubwa inayofanywa na waandishi wa habari katika kuuhabarisha umma wa
Watanzania ila amehimiza pia waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi, kanuni na taratibu.
Mjema ametoa kauli hiyo jana Dar es Salaam wakati wa
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari ambapo ametumia nafasi
hiyo kuelezea umuhimu wa vyombo hivyo katika maendeleo ya nchi yetu.
Maadhimisho
hayo yamefanywa na Jukwaa la Waandishi wa habari Mkoa wa Dar es Salaam
kwa kukutana na kujadili masuala ya mbalimbali yanayoikumba tasnia ya
habari.Kwa kukumbusha tu maadhmisho hayo duniani huadhimishwa kila
ifikapo Mei 2 na 3 ya kila mwaka.
Mjema
amehimiza pia waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia
weledi, kanuni na taratibu.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Waandishi wa habari
Jane Mihanji amesema wanahabari wanaomba kulindwa ili watekeleze
majukumu yao kwa uhuru zaidi.
Aidha changamoto ambazo zimeelezwa ikiwemo ya kukosa uhuru wa kufanya kazi ni vema nayo ikapatiwa ufumbuzi .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...