KITUO cha Utangazaji cha Efm redio katika kuhakikisha kinaenda sanjari na maendeleo pamoja na mpango wa serikali wa kuhamia Jijini Dodoma, imewasha rasmi masafa yake leo Jijini humo ambapo inasikika kupitia masafa ya 92.5 fm. 
Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa Efm Radio na TV E, Bwana Dennis Busulwa, wameelekeza matangazo ya kituo hicho Jiji la Dodoma kwa kuangalia uhitaji wa jamii pamoja na maendeleo ya jiji katika kuhabarisha, kuburudisha pamoja na kuelimisha.
Bwana Busulwa amesema Vilevile Efm redio inatarajia kuwasha masafa yake katika mkoa wa Morogoro, Tabora, na Kigoma pamoja na mikoa mingine ili kuhakikisha watanzania wote wanapata matangazo yake.
Aidha, Efm redio inazidi kuishukuru serikali na wadau wake wote hususani wasikilizaji wake kwa kuendelea kuwaunga mkono pamoja na kuwaahidi wasikilizaji wake kutimiza wajibu wake uliojiwekea kama chombo cha habari pamoja na kufikisha matamasha yake hususani ya uwezeshaji katika kuendeleza uchumi pamoja na elimu katika jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...