JENGO la kihistoria la Beit el ajab liliopo Forodhani Mjini Zanzibar linalotarajiwa kufanyiwa matengenezo makubwa na Serekali ya Oman baada ya kubomoka baadhi ya sehemu zake miaka michache iliyopita.
WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza katika hafla ya kumuaga Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk ( kushoto) iliyofanyika katika jengo la kihistoria la Beit el ajab Forodhani. Wa kwanza (kulia) Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Dkt. Amina Ameir na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Khadija Bakari Ali.
KATIBU MKUU Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk akizungumza na Viongozi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar kuhusu matengenezo makubwa ya Jengo la Beit el ajab ambalo lilibomoka miaka michache iliyopita, (kulia) Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo.
WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi zawadi mbalimbali Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk baada ya kumaliza ziara ya kutembelea Maeneo mbalimbali ya historia ya Zanzibar.
WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akiagana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk baada ya kumaliza ziara yake Zanzibar.
(Picha na Abdalla Omar Maelzo Zanzibar).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...