Waheshimiwa Majaji wapya wa Mahakama Kuu walioteuliwa kutoka Mahakama wakiwa katika picha ya pamoja, katikati ni Mhe. Ilvin Mugeta, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, kushoto ni Mhe. Elinaza Luvanda, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na aliyesimama kulia ni Mhe. Mustapher Siyani, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Majaji hawa wameagwa rasmi mapema Mei 04, 2018 na Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania.
Sehemu ya Wajumbe wa Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania wakiwa katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Maktaba-Mahakama ya Rufani, katika kikao hicho Wajumbe hao walipata fursa ya kuwaaga waliokuwa Wajumbe wa Menejimenti ambao waliteuliwa hivi karibuni kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, walioketi mbele (katikati) ni Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga, kulia ni Mwenyekiti Mwenza wa kikao hicho ambaye pia ni Msajili Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati na kushoto ni Msajili-Mahakama ya Rufani, Mhe. John Kahyoza.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ilvin Mugeta (aliyesimama) akitoa neno la shukrani kwa Wajumbe wa Menejimenti, katika salaam zake za shukrani, Mhe. Jaji Mugeta ameishukuru Menejimenti kwa ushirikiano katika kipindi chote alichofanya kazi katika nafasi ya Msajili-Mahakama Kuu, aidha; Mhe. Mugeta ameomba ushirikiano zaidi katika nafasi hii mpya.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Elinaza Luvanda akitoa neno la shukrani kwa Wajumbe wa Menejimenti, amemshukuru Mhe. Rais na Viongozi wengine wa Mahakama kwa uteuzi wa nafasi hiyo, na ameahidi kutoa ushirikiano katika kazi yake.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...