Nakala ya hukumu ni haki yako ikiwa ulikuwa mhusika katika
kesi au shauri. Unakuwa mhusika katika kesi au shauri pale unapokuwa mshitaki
au mshitakiwa, mlalamikaji au
mlalamikiwa, au mhusika mwingine mwenye maslahi. Hapa ndipo unapohesabika kuwa mhusika katika
kesi au shauri na hapa ndipo unapokuwa na haki ya kuomba kupatiwa nakala ya
hukumu.
Makala yaliyopita yalieleza kuwa nakala ya hukumu ni muhimu
hasa ukitaka kukata rufaa au kuchukua hatua zaidi , lakini pia ni muhimu kama
nyaraka ya kumbukumbu kwa ajili ya kesho, pia ni muhimu kwa ajili ya
utekelezaji wa kile kilichoamuliwa. Leo
tuone mfano halisi wa barua ya maombi
ya nakala ya hukumu
kama ulivyo hapa
chini ;-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,
24 / 5 / 2018
S.L.P..............................
Dar es salaam.
YAH ; MAOMBI YA KUPATIWA NAKALA YA
HUKUMU.
Nilikuwa mlalamikiwa katika shauri namba
13 la mwaka 2018, ambalo
limetolewa hukumu tarehe 22 / 3 / 2018, mbele ya Mhe. Kijana Mponela. Ninaomba
kupatiwa nakala ya hukumu kwa kumbukumbu
au hatua zaidi.
Wako
Mti Mkavu
( Aliyekuwa mlalamikiwa ).
0717600900
Sahihi...............................
KUSOMA ZAIDI sheriayakub.blogspot.com



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...