Na  Bashir Yakub.

Nakala ya hukumu ni haki yako ikiwa ulikuwa mhusika katika kesi au shauri. Unakuwa mhusika katika kesi au shauri pale unapokuwa mshitaki au mshitakiwa,  mlalamikaji au mlalamikiwa, au mhusika mwingine mwenye maslahi.  Hapa ndipo unapohesabika kuwa mhusika katika kesi au shauri na hapa ndipo unapokuwa na haki ya kuomba kupatiwa nakala ya hukumu.

Makala yaliyopita yalieleza kuwa nakala ya hukumu ni muhimu hasa ukitaka kukata rufaa au kuchukua hatua zaidi , lakini pia ni muhimu kama nyaraka ya kumbukumbu kwa ajili ya kesho, pia ni muhimu kwa ajili ya utekelezaji wa kile kilichoamuliwa.  Leo tuone mfano halisi wa barua ya  maombi ya  nakala ya hukumu 

kama ulivyo hapa chini ;-


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,                                                        24 / 5 / 2018
S.L.P..............................
Dar es salaam.
YAH ; MAOMBI YA KUPATIWA NAKALA YA HUKUMU.
Nilikuwa mlalamikiwa katika shauri namba  13 la mwaka 2018,  ambalo limetolewa hukumu tarehe 22 / 3 / 2018, mbele ya Mhe. Kijana Mponela. Ninaomba kupatiwa nakala ya hukumu  kwa kumbukumbu au hatua zaidi.
Wako
Mti Mkavu
( Aliyekuwa mlalamikiwa ).
0717600900
Sahihi...............................
               
  KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...