Na Ankal
Unapopiga picha ya ndege inayotumia pangaboi ni muhimu kuhakikisha kwamba kasi ya shata (shutter speed) ya kamera yako sio ya juu sana ama sivyo picha utayopata ni ya pangaboi kuonekana hazitembei wakati ndege ipo hewani, jambo ambalo litaua uhalisia wa picha.
Kwa kawaida kugandisha kitendo (action) ni jambo jema lakini kwa ndege picha itaonekana ya mgando na isiyo na afya. Yaani kama ndege ipo angani na pangaboi zimeganda itaonekana picha isiyotimia. Tatizo kwa wapiga picha wengi hasa wanaotumia simu, aghalabu wakati wa mchana kamera za simu huwa zinajitega kwenye “automatic’ hivyo shata inakuwa kwenye kasi kubwa. Kwa luigha ingine ni kwamba kasi ya shata ikiwa ndogo itaonesha mzunguko halisi wa pangaboi. 
 Hii imepigwa kwa kamera ya kawaida aina ya Canon EOS 5D Mark lll
Hii imepigwa kwa simu ya Iphone 7.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. The second picture is on upside down. The plane was on approaching landing with slow speed or landed already. U trick us Michuzi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...