Mwakilishi wa kampuni ya QNET Tanzania Andrew Gerald akikabidhi msaada wa vyakula wenye thamani ya 9mil/- kwa Mlezi wa kituo cha watoto wenye mahitaji maalum cha Maunga kilichopo Kinondoni Hananasif Dar Es Salaam, Bi. Zainab Bakary kwa ajili ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Kampuni ya QNET inatoa msaada kwa nchi mbali mbali 13 barani Afrika kwa ajili ya mfungo wa mwezi wa Ramadhani.
Wawakilishi wa kampuni ya QNET Tanzania wakikabidhi msaada wa vyakula wenye thamani ya 9mil/- kwa Mlezi wa kituo cha watoto wenye mahitaji maalum cha Maunga kilichopo Kinondoni Hananasif Dar Es Salaam, Bi. Zainab Bakary kwa ajili ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Kampuni ya QNET inatoa msaada kwa nchi mbali mbali 13 barani Afrika kwa ajili ya mfungo wa mwezi wa Ramadhani.
kampuni ya mauzo ya moja kwa moja
inayoongoza kwa kushirikiana na mwakilishi wake wa kijitegemea (IRs) kuleta
shangwe na faraja kwa jamii mbalimbali zisizojiweza katika kuashiria mwezi
mtukufu wa Ramadhan, katika nchi 13 za Kiafrika.
Kampeni hii ya mwaka ina lengo la kuboresha maisha ya wengi na inaenda
sambamba na falsafa ya kampuni hii ya (RYTHM) Jiinue kuwasaidia wanadamu
(Raise Yourself to Help Mankind) Mafunzo ya msingi ya (RYTHM) wakati wote
yamekuwa yanalenga katika kuongeza juhudi zaidi ya wajibu katika kujali wale
ambao hawana uwezo kwa kuwapatia mazingira mazuri ya kuishi kwaajili yao,
hasa watoto ambao ni alama ya kizazi chetu kijacho.
Kampeni ya mwaka huu ya Ramadhan katika Afrika itashuhudia ushirikiano
mkubwa miongoni mwa wafanyakazi wa QNET, wakala na Wawakilishi Binafsi
(IR) wakiunganisha jitihada zao katika kuandaa mfululizo wa mwezi mzima wa
shughuli za kutoa misaada katika nchi kama Ivory Coast, Togo, Cameroon,
Guinea, Burkina Faso, Tanzania, Niger, Uganda, Chad, Mali, Ghana and Senegal.
Nchini Tanzania, tukio la utoaji wa misaada ya Ramadhan litashuhudia utoaji
wa mchele, tambi, sukari na bidhaa zingine za chakula na matumizi kwa kituo
cha Kulelea watoto yatima cha Maunga Children Centre jijini Dar es salaam.
Kuna watoto 54 katika kituo cha kulelea watoto yatima cha
Maunga Children Centre ambacho kilianzishwa katika mwaka 2008. Makazi
haya ya watoto kwa sasa yanasimamiwa na Zainab Bakary na wanategemea
misaada ya umma na wasamaria wema kuweza kukabiliana na gharama za
mahitaji ya watoto ya vyakula na vinywaji.
Akizungumzia kuhusu tukio hilo mwaka huu, Trevor Kuna, CEO wa QNET,
amesema "Kampeni za kutoa misaada ya Ramadhan imekua moja kati ya
kampeni zetu za msingi za kila mwaka. Kwa kweli ni muhimu sana, inatia moyo
na inakamilisha jitihada za QNET. Kampeni kama hizi huhamasisha uwezeshaji
wa jamii na pia huwa zinahamasisha sana kwa wafanyakazi wetu na
Wawakilishi wetu binafsi (IR's) kwa kushiriki wao binafsi katika kuboresha
maisha ya engine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...