Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe pamoja Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy kushoto  na Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer kulia kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 katika sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Nyandeo Kidatu mkoani Morogoro. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli watatu kutoka kushoto pamoja viongozi mbalimbali na wabunge wa mkoa wa Morogoro.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi pamoja na viongozi wengine wakiwemo Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy anayevuta utepe, Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer pamoja na wabunge mbalimbali wa mkoa wa Morogoro
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer na Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy mara baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 katika sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Nyandeo Kidatu mkoani Morogoro.
Mbunge wa Mikumi Joseph Haule akitumbuiza mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara yenye jumla ya kilometa 66.9 pamoja na daraja la mto Ruaha lenye urefu wa mita 130.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kwa njia ya simu ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo kuhusu matatizo ya mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa maji katika kata ya  Kidodi mkoani Morogoro.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...