Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendeleza utaratibu wake wa kutoa elimu zaidi juu ya sekta ya gesi asilia na mafuta kwa wadau mbalimbali safari hii ikiwa ni kwa viongozi wa dini kutoka Mkoa wa Lindi. Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea kiwanda cha kuchakata gesi asilia cha Madimba, Meneja Mawasiliano wa TPDC, Bi. Marie Msellemu alisema “huu ni muendelezo wa mikakati ya Shirika katika kujenga uelewa na mahusiano bora na wadau ambapo leo hii tupo na viongozi wa dini kutoka katika vijiji na mitaa linapopita bomba la gesi kwa Mkoa wa Lindi”. 

Bi. Msellemu alieleza kwamba, TPDC akiwa kama shirika la mafuta la Taifa linalo jukumu sio tu la kuzalisha na kusambaza gesi asilia bali pia kuhakikisha elimu sahihi juu ya manufaa na faida za miradi ya gesi asilia inapatikana kwa wadau wote. Bi. Msellemu alifafanua kwamba, TPDC iliona ni vema kuwajengea uelewa zaidi viongozi wa dini kwani wao ni nguzo muhimu katika jamii na pia ni watu wenye ushawishi mkubwa hivyo kuelewa kwao juu ya maendeleo ya sekta ya gesi asilia na mafuta kutasaidia kusambaza uelewa zaidi kwa waumini wao. 

Ziara ya viongozi wa dini kutoka Mkoani Lindi haikuishia katika kutembelea kiwanda cha kuchaka gesi asilia pekee bali pia walipata fursa ya kusikiliza mada kuhusiana na maendeleo katika mkondo wa juu na mkondo wa chini katika sekta ya mafuta na gesi asilia. Mada hizi zilitolewa na wataalamu kutoka TPDC ambapo, Ndg. Shaidu Nuru, Mjilojia kutoka TPDC alitoa mada kuhusu maendeleo katika mkondo wa juu na kugusia hali ya utafiti nchini kwa sasa na maendeleo katika mradi mkubwa wa LNG. Akitoa mada hiyo, Ndg. Shaidu alisema “ utafiti wa mafuta na gesi asilia nchini ni zoezi endelevu ambalo limepelekea ugunduzi mkubwa wa shehena ya gesi asilia (futi za ujazo 57.83 trilioni) katika nchi kavu na kina kirefu cha bahari”.
 Viongozi wa dini kutoka mkoani Lindi wakitembelea kiwanda cha kuchakata gesi asilia, Madimba-Mtwara
Maalamu kutoka TPDC, Godbless Swagarya akifafanua jambo kwa viongozi wa dini walipotembelea kiwanda cha kuchakata gesi asilia cha Madimba, Mtwara. 
Sehemu ya viongozi wa dini kutoka Lindi wakiwa katika ziara ya kutembelea kiwanda cha kuchakata gesi asilia cha Madimba, Mtwara. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...