Dkt, Mahiga afungua Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania, Israel

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amezindua rasmi ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Israel na kuitaka Israel nayo iharakishe kufungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania. 

Ufunguzi wa ofisi hiyo ya ubalozi iliyopo katika mji wa Tel Aviv ulifanyika leo na ulihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Ayelet Shaked, Mabalozi wa nchi za Afrika na Watanzania wanaoishi nchini humo.

Katika hotuba yake, Dkt. Mahiga aliitaja Israel kama nchi ya kupigiwa mfano kwa sababu licha ya changamoto za kimahusiano na baadhi ya jirani zake lakini bado nchi hiyo imepiiga hatua kubwa za kimaendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo cha umwagiliaji, viwanda, matibabu, TEHAMA, ulinzi na usalama, uhifadhi wa maji na masuala ya nishati ikiwemo nishati ya kutumia joto ardhi.

Kwa upande wa ulinzi na usalama, Waziri Mahiga alisema Watanzania hawataisahau Israel kwa kuwa ndiyo nchi iliyoisaidia Tanzania kuanzisha Jeshi la Kujenga Taifa ambalo mafanikio na mchango wa jeshi hilo unajulikana na kila Mtanzania. Alisema JKT baada ya lugha ya Kiswahili ndiyo chombo cha pili kilichosaidia kwa kiasi kikubwa kuunganisha makabila zaidi ya 120 ya Watanzania na kuwa wamoja hadi leo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akikata utepe kuashiria ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel Ufunguzi huo ulifanyika jijini Tel Aviv tarehe 08 Mei 2018. Wengine katika picha ni Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima.wakigongesheana glasi kwa ajili ya kuwatakia afya njema viongozi wa mataifa yao, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga wakisalimiana na Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked walipowasili kwa ajili ya kushiriki ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afriika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiweka saini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili kwenye ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel kwa ajili ya kuzifungua rasmi. Anayemwangalia ni Waziri wa Sheria wa Israel, Mhe. Bibi Ayelet Shaked .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...