Na Mwandishi wetu.

VYOMBO vya habari nchini vimekumbushwa kwamba uhuru wa habari sio kuiangalia tu serikali, bali kujiangalia  wenyewe na pia vyombo vyao vya habari.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe wakati akihutubia hadhira ya waandishi wa habari katika kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani, sherehe zilizofanyika kitaifa katika hoteli ya Morena Jijini Dodoma.

Katika hotuba yake baada ya kusikiliza hoja kadha kutoka taasisi mbalimbali kuhusiana na uhuru wa vyombo vya habari nchini na hisia kwamba vinaminywa Waziri huyo alisema kwamba ipo haja ya tasnia kujiangalia yenyewe kama inatenda haki na weledi kwa taifa hili.
“Kalamu ya mwanahabari ina nguvu sana, ina nguvu sawa na ya silaha, ikitumiwa vizuri ni mlinzi na ikitumiwa vibaya ni maafa” alisema Dk. Mwakyembe.

Alisema katika mazingira ya sasa ambako kuna walimu wengi kuna baadhi ya watu wanapiga kelele kuhusu kufuatwa kwa sheria wakisema sio demokrasia, huku wakifahamu fika kwamba hata katika nchi zao hicho wanachoimba demokrasia hakipo.Akihutubia kama mgeni rasmi alisema kwamba ingawa dirisha lipo wazi kwa majadiliano, serikali haitarudi nyuma kutokana na haja mahsusi ya udhibiti wa yanayoendelea katika mitandao kwa manufaa ya taifa hili leo na kesho.

 “Kuhusu Kanuni za Maudhui Mtandaoni, hili tunaweza kukaa na kujadili lakini kama Serikali hatutarudi nyuma katika hili. “Kupitia mtandao, bila kuweka udhibiti kuna mambo mengi yanapita ambayo hatuwezi kukubaliana nayo”  alisema Dk Mwakyembe.

Akiwasilisha salamu za Jukwaa la wahariri nchini TEF, Kaimu Mwenyekiti Deodatus Balile alisema kwamba ipo haja ya kuendesha mdahalo wa kitaifa kuhusu mustakabali wa uhuru wa habari nchini Tanzania ambao hatima yake ni amani na maridhiano.
 Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza kwenye kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit, akitoa salamu za Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Audrey Azoulay wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Naibu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Charles Stuart akitoa salamu za Umoja huo wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakfu wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Fausta Musokwa akitoa salamu za TMF wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

 Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Edda Sanga akitoa salamu za taasisi hiyo wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
  Afisa Programu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Paul Mallimbo akitoa salamu za Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Kajubi Mukajanga wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Jane Mihanji akitoa salamu za UTPC wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit akimkabidhi Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe nakala ya ripoti inayohusu uhuru wa kujieleza na maendeleo ya vyombo vya habari wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Katikati anayeshuhudia tukio hilo ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari.
 Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akisalimiana na Mtaalamu wa Masuala ya Vyombo vya Habari na Mkufunzi wa Kujitegemea, Rose Haji Mwalimu wakati wa kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mkuu wa wilaya ya Kongwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Deogratius Ndejembi akizungumza na washiriki wakati akifunga kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari wakongwe (Veterans) mara baada ya kuhutubia kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...